Twitter yaondoa karibu akaunti 3,500 za propaganda 'zinazoungwa mkono na serikali'


Twitter inasema imeondoa akaunti 3,465 zinazofanya kazi kama "operesheni za habari zinazoungwa mkono na serikali" ambazo ilizihusisha na nchi sita: Uchina, Mexico, Urusi, Tanzania, Uganda na Venezuela.


Nchini Uganda, Twitter iliondoa mtandao wa akaunti 418 "zilizokuwa zikishiriki katika shughuli zisizo halali" za kumuunga mkono Rais Yoweri Museveni na chama chake, National Resistance Movement.


Takriban akaunti 270 pia zilifungwa nchini Tanzania baada ya kupatikana kuwasilisha ripoti za nia mbaya kwenye Twitter, zikiwalenga wanachama na wafuasi wa FichuaTanzania, kikundi cha kutetea haki za kiraia.



Comments

Popular posts from this blog

NINATIBU KISUKARI, PRESHA, TEZIDUME, NGIRI NA NGUVU ZA KIUME

Uchaguzi wa rais nchini Libya uko mashakani

Mambo 8 yanayosababisha Gari kuwaka Moto na Jinsi ya kuyaepuka