Miili 9 zaidi yapatikana baada ya tukio la kuzama kwa boti Nigeria


 Maafisa wa Nigeria wamethibitisha kuwa miili tisa zaidi ya mkasa wa ajali ya boti ya Jumanne imepatikana Jumatano asubuhi.


Hii inafanya idadi ya waliofariki kufikia 29 kufikia sasa.


Shughuli ya utafutaji na uokoaji inaendelea ikihusisha polisi, zima moto na wanachama wa Kikosi cha Usalama na Ulinzi wa Raia wa Nigeria pamoja na waliojitolea.


Polisi katika eneo hilo wameiambia BBC kwamba idadi ya manusura waliookolewa kufikia sasa bado ni saba.


Manusura wa ajali ya boti walikuwa wengi wanafunzi wa shule ya Kiislamu - wenye umri wa kati ya miaka sita na 12 - waliokuwa wakisafiri kwenda kwenye sherehe za kidini katika mji wa Bagwai.



Comments

Popular posts from this blog

NINATIBU KISUKARI, PRESHA, TEZIDUME, NGIRI NA NGUVU ZA KIUME

Uchaguzi wa rais nchini Libya uko mashakani

Mambo 8 yanayosababisha Gari kuwaka Moto na Jinsi ya kuyaepuka