Biden amuonya Putin huku kukiwa na hofu ya uvamizi wa Ukraine

 


Marekani imesema inajitayarisha na "majibu makali" kutokana na hofu ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, baada ya mazungumzo ya Rais Biden na Vladimir Putin.


Katika video, Bw Biden alionesha wasiwasi mkubwa juu ya kuongezeka kwa wanajeshi wa Urusi na kutishia "hatua kali za kiuchumi na zingine", Washington ilisema.


Urusi yasema haitaishambulia Ukraine.

Bw Putin alishutumu Kyiv kwa uchochezi, na akataka hakikisho dhidi ya upanuzi wa Nato wa mashariki na kupelekwa kwa silaha za kukera karibu na Urusi.


Walizungumza kwenye kiunga salama cha video kilichowekwa chini ya tawala zilizopita lakini hazikuwahi kutumika hapo awali, shirika la habari la Urusi Tass lilisema.


Picha za video za matukio ya ufunguzi zilionesha salamu za kirafiki kati ya viongozi wa Marekani na Urusi.


Mazungumzo hayo yakaendelea nyuma ya milango iliyofungwa, iliyochukua muda wa saa mbili.


Bw Putin alifanya mazungumzo hayo kutoka katika makazi yake katika eneo la mapumziko la kusini la Sochi, kulingana na Tass.



Comments

Popular posts from this blog

NINATIBU KISUKARI, PRESHA, TEZIDUME, NGIRI NA NGUVU ZA KIUME

Uchaguzi wa rais nchini Libya uko mashakani

Mambo 8 yanayosababisha Gari kuwaka Moto na Jinsi ya kuyaepuka