Waziri wa Mambo ya Ndani wa kwanza mwanamke wa Msumbiji ateuliwa

 


Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi amemteua Arsenia Felicidade Felix Massinge kuwa waziri wa kwanza mwanamke wa Mambo ya Ndani nchini humo.


Pia amemteua waziri mpya wa ulinzi wa taifa, Cristóvão Artur Chume.


Mawaziri waliopita waliohusika na ulinzi na usalama wa ndani wote walifutwa kazi wiki hii.


Bw Chume ni Meja Jenerali anayejulikana kwa kuongoza vikosi vilivyokomboa miji mingi, ikiwa ni pamoja na Mocimboa da Praia katika jimbo la Cabo Delgado lililoathiriwa na wanajihadi.


Bi Massinge kabla ya kuteuliwa kwake alikuwa Kamishna Mkuu wa Uhamiaji.


Pia amefanya kazi huko nyuma kama Kamanda wa Polisi wa mkoa katika mikoa ya Inhambane, Manica na Nampula.


Anatarajiwa kutumia uzoefu wake serikalini kukabiliana na changamoto nyingi zinazomkabili mtangulizi wake - ikiwa ni pamoja na ugaidi, ufisadi na utekaji nyara.



Comments

Popular posts from this blog

NINATIBU KISUKARI, PRESHA, TEZIDUME, NGIRI NA NGUVU ZA KIUME

Uchaguzi wa rais nchini Libya uko mashakani

Mambo 8 yanayosababisha Gari kuwaka Moto na Jinsi ya kuyaepuka