Watu 43 wauawa katika mapigano ya kikabila Sudan


Umoja wa Mataifa umethibitisha kuwa katika siku kadhaa za mapigano ya jamii katika jimbo la Darfur nchini Sudan yamesababisha takriban watu 43 kupoteza maisha na maelfu kuyahama makazi yao.


Mzozo huo ulizuka wiki iliyopita kati ya wafugaji wahamaji wa Kiarabu na wakulima kutoka kabila la Misseriya Jebel, huko Jebel Moon, magharibi mwa Darfur.


Umoja wa Mataifa unasema zaidi ya vijiji 40 vilichomwa moto na kuporwa katika mapigano hayo.


Watu kadhaa wameripotiwa kupotea wakiwemo watoto.


Kumekuwa na milipuko ya mara kwa mara ya ghasia huko Darfur tangu kusainiwa kwa mkataba wa amani mwishoni mwa mwaka jana ambao ulisababisha kuondolewa kwa walinda amani wa Umoja wa Mataifa.



Comments

Popular posts from this blog

NINATIBU KISUKARI, PRESHA, TEZIDUME, NGIRI NA NGUVU ZA KIUME

Uchaguzi wa rais nchini Libya uko mashakani

Mambo 8 yanayosababisha Gari kuwaka Moto na Jinsi ya kuyaepuka