Watu 20 wauawa katika shambulizi la wanamgambo nchini Burkina Faso


Takriban watu 20 wameuawa katika shambulizi la wanamgambo katika eneo la mpaka wa kaskazini mwa Burkina Faso, mamlaka imesema.


Kumi na tisa kati ya wahasiriwa wanasemekana kuwa maafisa katika jeshi la polisi na mmoja alikuwa raia.


Wanamgambo hao walilenga ngome karibu na mgodi wa dhahabu huko Inata.


Siku mbili kabla maafisa saba wa polisi waliuawa katika shambulio jingine katika eneo hilo, ambalo linapakana na Mali na Niger.


Wanamgambo wa Kiislamu wenye uhusiano na al-Qaeda na kundi la Islamic State wanafanya kazi katika eneo la mpakani.


Nchi hizo tatu, zikisaidiwa na Chad na Ufaransa, zimetuma mamia ya wanajeshi huko.



Comments

Popular posts from this blog

NINATIBU KISUKARI, PRESHA, TEZIDUME, NGIRI NA NGUVU ZA KIUME

Uchaguzi wa rais nchini Libya uko mashakani

Mambo 8 yanayosababisha Gari kuwaka Moto na Jinsi ya kuyaepuka