Wanafuzi 25 wapata mimba Rukwa


 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti ameagiza Wakuu wa Wilaya za mkoa huo kuhakikisha wanafuatilia na kudhibiti kuongezeka kwa wanafunzi wa kike wanaokatisha masomo kutokana na tatizo la mimba ambapo kwa mwaka 2021 matukio 25 ya wanafunzi wa kike kupewa mimba yameripotiwa.


Akizungumza mjini Sumbawanga Mkuu huyo wa Mkoa alionesha kutofurahishwa na kasi ya kuongezeka kwa wanafunzi wa kike wanaoshindwa kukamilisha masomo yao sababu ikitajwa kuwa ni kupata ujauzito.


“Lazima tuongeze mapambano kudhibiti mimba za utotoni .Sijafurahishwa kuona wilaya ya Nkasi ikiwa na idadi ya wanafunzi Ishirini Tano (25) mwaka huu waliopata mimba wakiwa wanasoma. Hii haikubaliki. Wakuu wa wilaya nendeni mkadhibiti vitendo hivi” alisisitiza Mkirikiti.


Takwimu za Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa zimeonesha kuwa katika mwaka huu 2021 wilaya ya Nkasi imekuwa na matukio 25 ya wanafunzi wa kike kupata mimba huku wilaya ya Kalambo ikiripoti wasichana wanane (8) na Wilaya ya Sumbawanga nayo ikiwa na wanafunzi wanane (8).



Comments

Popular posts from this blog

NINATIBU KISUKARI, PRESHA, TEZIDUME, NGIRI NA NGUVU ZA KIUME

Uchaguzi wa rais nchini Libya uko mashakani

Mambo 8 yanayosababisha Gari kuwaka Moto na Jinsi ya kuyaepuka