Sudan yarejesha huduma za intaneti huku maandamano ya kupinga mapinduzi yakiendelea
Mamlaka za Sudan zimerejesha mtandao wa intaneti karibu mwezi mmoja tangu usitishwe baada ya jeshi kuondoa serikali ya mpito inayoongozwa na raia.
Kampuni zote za mawasiliano zilirejeshewa huduma zao za mtandao siku ya Alhamisi.
Mahakama ilikuwa imeamuru kampuni tatu kuu za mawasiliano nchini humo kurejesha intaneti mnamo tarehe 9 Novemba, lakini tatizo hilo liliendelea.
Kituo cha kuchunguza uhuru wa mtandao, Netblocks, pia kimethibitisha kurejeshwa kwa huduma hizo.
"Imethibitishwa: Mtandao umerejeshwa kwa kiasi nchini #Sudan siku ya 25 ya kukatika baada ya mapinduzi; vipimo vya wakati halisi vinaonyesha ongezeko kubwa la muunganisho wa simu za mkononi kutoka 4:30 jioni saa za ndani; haijulikani ikiwa huduma itahifadhiwa, au kwa muda gani. ," ilisema kwenye akaunti yake rasmi ya Twitter.
Maandamano mabaya ya kupinga mapinduzi yamekuwa yakifanyika katika mji mkuu Khartoum na maeneo mengine ya Sudan tangu Jenerali Abdel Fattah al-Burhan achukue mamlaka tarehe 25 Oktoba. Zaidi ya watu 30 wameripotiwa kuuawa katika maandamano hayo.
Wanaharakati na makundi ya upinzani wamefaulu kuangazia maandamano hayo kwenye mitandao ya kijamii licha ya kuwekewa vikwazo.
Akaunti rasmi ya Facebook ya Wizara ya Habari, ambayo inaambatana na Waziri Mkuu aliyeondolewa madarakani Abdalla Hamdok, pia imekuwa na sauti dhidi ya watawala wa kijeshi.
Comments
Post a Comment