Mabomu mawili yalipuka Kamapala

 


Mabomu mawili yamelipuka leo Jumanne Novemba 16, 2021 katika Jiji la Kampala nchini Uganda.


Taarifa kutoka Kampala zinasema kuwa bomu moja limelipuka mkabala na Kituo Kikuu cha Polisi katika Jiji la Kampala jingine lililipuka karibu na jengo la Bunge la Uganda.


Kutokana na milipuko hiyo, Bunge la Uganda limezingirwa na vyombo vya ulinzi na usalama.


Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Uganda, baadhi ya watu wamejeruhiwa kutokana na milipuko hiyo.


Picha na video ambazo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha moshi mzito umetanda huku baadhi ya magari yakionekana yakiwa yanateketea kwa moto.



Comments

Popular posts from this blog

NINATIBU KISUKARI, PRESHA, TEZIDUME, NGIRI NA NGUVU ZA KIUME

Uchaguzi wa rais nchini Libya uko mashakani

Mambo 8 yanayosababisha Gari kuwaka Moto na Jinsi ya kuyaepuka