Posts

Showing posts from August, 2021

Unaambiwa Mbunge wa CCM aliyejiuzulu afunguka Makubwa

Image
  Mbunge aliyejiuzulu afunguka TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa Jimbo la Konde visiwani Zanzibar lipo wazi na taratibu za kujaza nafasi hiyo zitatangazwa hivi karibuni. Hayo yalibainishwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC Dk Wilson Mahera kupitia taarifa yake kwa umma jana. Dk Mahera alisema NEC ilipokea barua kutoka kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ikitaarifa kuwa, Mbunge Mteule wa Jimbo la Konde, Sheha Mpemba Faki, alikitaarifu chama hicho kuwa hayupo tayari kuwawakilisha wananchi wa Jimbo la Konde kutokana na changamoto za kifamilia. Alisema kutokana na hilo, NEC inautaarifu umma kuwa jimbo hilo lipo wazi na taratibu za kujaza nafasi hiyo zitatangazwa. “Tume ifanya hivyo kwa kuwa ilikuwa bado haijamjulisha Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kuhusu kukamilika kwa uchaguzi katika Jimbo la Konde na kuchaguliwa kwa Mbunge huyo Mteule. Pia Tume ilikuwa haijamtangaza kwenye Gazeti la Serikali kama ilivyoelekezwa katika Kifungu cha 81 (c) cha Sheria ya Taifa y...

Kunani Wasafi... Mtangazaji Maulide Kitenge Awakimbia...Wasafi FM Waandika Haya

Image
  Kwa Dhati Kabisa Tunatoa Shukrani za Dhati kwa mchango wako mkubwa Katika taasisi yetu ya #WasafiMedia kwa kuwa nasi bega kwa bega kuanzia Media changa mpaka leo imekuwa Media Namba Moja Nchini Mbali ya ushiriki wako kwenye Media umetufundisha mengi na kutuonesha njia nzuri zaidi ili kutimiza Malengo ya WASAFI MEDIA kuwa chombo kikubwa cha Habari Africa na kulipa Heshima Taifa letu...🇹🇿 @mauldikitenge #KochaMchezaji #Kwaheri #AsanteTunashukuru

Watatu wasimamishwa kazi, Kamati yaundwa kuchunguza moto Msamvu

Image
  Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amewasimamisha kazi wahandisi watatu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kupisha uchunguzi baada ya Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme Msamvu kuungua moto na kusababisha hasara ya takribani shilingi Bilioni 2. Aidha amemuagiza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Kheri Mahimbali kuunda kamati ya kuchunguza na kubaini chanzo halisi cha Moto huo na hasara iliyopatika ndani ya siku tano kuanzia leo (Agosti 3, 2021). Katika ziara hiyo, Dkt. Kalemani aliambatana na Naibu  Katibu Mkuu wizara hiyo, Kheri Mahimbali, Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Edward Ishengoma, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt.Tito Mwinuka pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Wizara na TANESCO. Sambamba na hilo aliiagiza Kampuni ya inayotekeleza Mradi wa Reli ya Umeme (SGR) kumchungumza mhandisi wake anayedaiwa kusababisha hitilafu hiyo kwa kukata waya wa umeme na kari la kuchimbua barabara wakati akitekeleza majukumu yake na kuchukuliwa hatua pindi itakapob...

Mfanyabiashara Ndama Ahukumiwa Kulipa Dola 75,000

Image
  Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu mfanyabiashara maarufu nchini,  Ndama Shabani ‘Ndama mtoto wa Ng'ombe’ na mwenzake Yusuph Yusuph kulipa fidia ya dola za kimarekani 75,000 kwa malalamikaji Emanuel Motilhathedi baada ya kupatikana na hatia ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu. Washtakiwa hao wanadaiwa kujipatia dola za kimarekani 150, 000 kutoka kwa mlalamikaji huyo ambaye ni raia wa Botswana kwa madai kuwa wangemuuzia kilo 500 za dhahabu lakini hawakufanya hivyo. Hukumu hiyo imetolewa leo,  Jumatatu Agosti 2, 2021 na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Godfrey Isaya baada ya washtakiwa hao kukiri mashtaka, kupitia majadiliano baina yao na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini ( DPP).

Olimpiki Tokyo 2020: Mganda Joshua Cheptegei ashinda dhahabu katika mbio za mita 5,000

Image
  Joshua Cheptegei wa Uganda alishinda medali yake ya pili kwenye Olimpiki ya Tokyo wakati aliponyakua dhahabu ya mbio za 5,000m ili kuiongeza na medali ya fedha alioshinda katika mbio za mita 10,000. Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 24 alimaliza mbele ya Mzaliwa wa Somalia raia wa Canada Mohammed Ahmed, ambaye alishinda fedha, na mzaliwa wa Kenya Mmarekani Paul Chelimo, ambaye alichukua shaba kuiunganisha na fedha yake kutoka Michezo ya Rio. Cheptegei anakuwa raia wa kwanza wa Uganda katika historia kushinda medali mbili za Olimpiki baada ya kushinda fedha katika mita 10,000 za wanaume wiki moja iliyopita. Chelimo wa Marekani alijirusha utepeni kumnyima Mkenya Nicholas Kipkorir Kimemi medali ya shaba . Jacob Kiplimo wa Uganda, ambaye alikuwa mshindi wa medali ya shaba katika mita 10,000, alikuwa wa tano na mwenzake Oscar Chelimo alimaliza katika nafasi ya mwisho wakati Milkesa Mengesha wa Ethiopia alikuwa wa 10.